Nimezaliwa na kukulia Shaurimoyo, nikasoma shule za hapa, na nimejitoa kwa moyo wote kuwatumikia wananchi. Safari yangu ya kazi imepita kwenye benki, bima, usafirishaji, na uongozi wa michezo. Nawakilisha Jimbo la Shaurimoyo kwa uadilifu na dhamira thabiti.
Mwananchi wa kawaida wa Shaurimoyo, Zanzibar ni muda mrefu nilikuwa mbali na nyumbani kwa ajili ya majukumu ya Kitaifa lakini moyo wangu haukuacha kudundia nyumbani nilipotokea, hii ndio Mitaa yangu, nyumbani kwangu na ni sehemu ambapo Moyo wangu umependezwa napo. Unaweza kunitoa Nje ya Shaurimoyo ila hauwezi kuitoa Shaurimoyo ndani yangu, kwa moyo mmoja na upendo mkubwa nimerudi nyumbani kwa ajili ya kuwatumikia Wananchi wenzangu.
Copyright ©2025 Arafat Ali Haji - MP for Shauri Moyo All Rights Reserved.